Ajali Dar Free Market usiku huu

NA DIRAMAKINI

WAKAZI wa Jiji la Dar es Salaam wamesema kuwa,ni jukumu la kila mwendesha chombo cha moto barabarani kuhakikisha anazingatia kanuni na taratibu za usalama barabarani ili kuepusha ajali za mara kwa mara ambazo licha ya kusababisha vifo, majeruhi, uharibifu wa vyombo vya moto pia ni moja wapo ya chanzo kikuu cha kuvutia umaskini.
Wameyasema hayo usiku wa kuamkia leo Mei 4, 2022 wakati wakizungumza na DIRAMAKINI BLOG muda mfupi baada ya ajali iliyotokea karibu na Dar Free Market katika Barabara ya Ali Hassan Mwinyi jijini Dar es Salaam.

Ajali hiyo ambayo imehusisha magari kadhaa kutokana na kutoelewana baina ya madereva huku kila mmoja akijiona yeye ndiye mwenye haki zaidi ya mwingine, ingawa haijasababisha vifo au majeruhi, lakini imesababisha uharibifu wa vyombo hivyo vya moto.
"Suala la usalama barabarani ni la muhimu sana, kwani tukiendelea kupuuzia jambo hili, hatuwezi kuyafikia malengo yetu ya maendeleo kama familia, jamii au Taifa. Ajali zinasababisha maafa makubwa, watu wanapoteza ndugu zao, viungo vinakatika, fedha zinatumika kwa ajili ya kugharamia matibabu, kuvirejesha vyombo vya moto vilivyoharibika katika hali yake ya awali.

"Hii kiuchumi inaashiria nini? Inaashiria tukishindwa kuzuia au kuzingatia kanuni za usalama barabarani kamwe hatutaweza kupata maendeleo endelevu, nitumie muda huu kuwashauri wenzangu, tuheshimu sheria za usalama barabarani, kwa kufanya hivyo tutakuwa tumeipa heshima familia, jamii na Taifa.
"Gharama zinazopaswa kutumika kwa ajili ya kugharamia majeruhi au kwa namna nyingine ile zitatumika kwa shughuli nyingine za maendeleo,"amesema Amos Justine mkazi wa Jiji la Dar es Salaam ambaye amezungumza na DIRAMAKINI muda mfupi baada ya kutokea ajali hiyo.

Kwa upande wake,Munira amesema kuwa,ni jukumu la kila mmoja kuhakikisha anazingatia usalama barabarani kwani, inapotokea ajali mara nyingi huwa yanajitokeza mambo ya ovyo.

"Kuna mambo ya ovyo ovyo ambayo ajali ikitokea huwa yanajitokeza mfano kutoleana lugha chafu, wengine kama hao unaowaona hapo si wote ni wema, wanaangalia namna ya kupata upenyo ili walau wapate chochote kitu humo ndani (udokozi), hivyo tukiwa barabarani tuhakikishe tunazingatia suala la usalama barabarani,"anasema Munira.

HIZI HAPA NAMBA ZA MAKAMANDA WA POLISI NA WAKUU WA USALAMA BARABARANI KWA MIKOA YA TANZANIA BARA;

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news