🔴LIVE:TCRA ikitoa ufafanuzi kuhusu huduma za Data nchini

NA DIRAMAKINI

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imetaja mabadiliko ya teknolojia na kwa gharama za data Tanzania iko chini kwa ukanda wa Jumuiya ya nchi zilizo Kusini Mwa Jangwa la Sahara na Ukanda wa Afrika mashariki.

Kupanda kwa gharama za matumizi ya Data za Internet kunatokana na mabadiliko ya uwekezaji wa miundombinu mbalimbali katika sekta ya mawasiliano lakini watoa huduma wameendelea kutoa huduma kulingana na matakwa ya kisheria na kufatiliwa na mamlaka ya udhibiti TCRA

Akizungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Masuala ya Kisekta TCRA, Dk. Emmanuel Manase alisema kuwa vifaa vya mawasiliano vinatengenezwa na kampuni chache duniani na kwamba bei ya vifaa hivyo, haiangalii uchumi wa nchi husika.

Alisema gharama za data mpaka Aprili mwaka huu ni kutoka Sh 1.67 hadi 2.60 huku bei ya data ikiwa Sh 1.5 kwa Megabaiti (Mb) hadi Sh 9.35 kwa Mb.

Dk. Manase amesema kuwa ili watanzania wote waweze kupata huduma hizo za data, uwekezaji mkubwa unahitajika ili nchi nzima ipate mawasiliano bila kujali uchumi na idadi ya watu.

"Stadi za TCRA zimeonesha kuwa gharama halisi za kuuza data ni kati ya Sh 2.03 Mb ambazo mtoa huduma anaweza kuuza na kurudisha gharama za uendeshaji na Sh 9.35 Mb ni ambazo mtoa huduma anaweza kuendeleza uwekezaji," alisema.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news