Simba SC yapigwa faini ya milioni 22.8/- kwa tuhuma za 'uchawi' uwanjani

NA DIRAMAKINI

SHIRIKISHO la Soka barani Afrika (CAF) limeipiga faini ya dola za Kimarekani 10,000 (zaidi ya shilingi milioni 22.8) Klabu ya Simba ya jijini Dar es Salaam, Tanzania.

Ni baada ya kupatikana na hatia kuwasha moto katika uwanja wa Orlando katika mchezo dhidi ya Orlando Pirates.
Kabla ya mchezo huo wa marudiano wa Kombe la Shirikisho,wachezaji wa Simba walionekana kukusanyika katikati ya uwanja na baadaye moshi kutokea katikati ya kundi hilo.

Taarifa kutoka CAF imesema, maafisa wa mchezo walionesha katika ripoti zao kwamba, wachezaji wa Simba waliwasha moto katikati ya uwanja wakati wakijifanya kuomba kabla ya mechi.

"Ilitubidi kumwaga maji ili kuuzima moto,”wameeleza huku wakibainisha kuwa, malipo hayo yanapaswa kufanyika ndani ya siku 60 kuanzia sasa.

MATOKEO Simba SC vs Orlando Pirates, April 23,2022, Robo Fainali CAF Confederation Cup 2021

Orlando Pirates Football Club is a South African professional football club based in the Houghton suburb of the city of Johannesburg and plays in the top-tier system of Football in South Africa known as Premier Soccer League, The team plays its home matches at Orlando Stadium in Soweto.
Simba Sports Club is a football club based in Kariakoo, Dar es Salaam Tanzania, Founded in 1936, the club was called Queens and later changed their name to Eagles, then to Sunderland. In 1971 they were renamed Simba. Simba is one of the two biggest clubs in Tanzania, alongside cross-city rivals Young Africans, Simba SC vs Orlando Pirates, Simba vs Orlando.

Orlando Pirates wamefuzu hatua ya Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika (CAF Confederation Cup) kwa mikwaju ya Penati 4-3 dhidi ya Simba SC.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news