Iringa rasmi umeme kidigitali

NA DIRAMAKINI

MKUU wa Mkoa wa Iringa, Mheshimiwa Queen Cuthbert Sendiga amezindua matumizi ya App ya Nikonekt ambayo inamwezesha mwananchi kuunganishiwa umeme kidigitali.
“Napenda kutoa pongezi kwa TANESCO (Shirika la Umeme Tanzania) mkoani Iringa kwa kuwajali wananchi wake na kuwarahisishia huduma zaidi kwa kuwapa nafasi ya kuunganishiwa na umeme wakiwa na simu yao kiganjani bila kufika katika ofisi za TANESCO kama ilivokuwa awali,"amesema Mheshimiwa Sendiga.

Aidha, mbali na pongezi nyingi alizozitoa Mheshimiwa Sendiga pia alitoa wito kwa wananchi kuendelea kutunza miundombinu ya umeme ili kuepusha gharama zisizokuwa za lazima katika kufanya matengenezo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news