Rais Dkt.Mwinyi awaapisha viongozi aliowateua

NA MWANDISHI DIRAMAKINI

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi amewaapisha viongozi mbalimbali aliowateuwa  Julai 10, 2021 kushika nyadhifa tofauti katika wizara za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi akimuapisha Nd.Mussa Haji Ali kuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Ikulu katika hafla iliyofanyika leo ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.
Mussa Haji Ali akila kiapo mbele ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) kuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Ikulu, katika hafla iliyofanyika leo ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.
Issa Mahfoudh Haji akila kiapo mbele ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) kuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa,Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ katika hafla iliyofanyika leo ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.

Katika hafla hiyo iliyofanyika Ikulu jijini leo Julai 12, 2021 Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, Dkt. Mwinyi alimuapisha Mussa Haji Ali kuwa Katibu Mkuu (OR), Ikulu pamoja na  Issa Mahafoudh Haji kuwa Katibu Mkuu (OR) Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ.

Wengine ni  Dkt. Habiba Hassan Omar kuwa Katibu Mkuu (OR) Kazi, Uchumi na Uwekezaji na Mikidadi Mbarouk Mzee kuwa Naibu Katibu Mkuu (OR) Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ.

Aidha, alimuapisha Aboud Hassan Mwinyi kuwa Naibu Katibu Mkuu (OR) Fedha na Mipango anayeshughulikia Fedha na Mipango.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi akimuapisha Nd.Issa Mahfoudh Haji kuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa,Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ katika hafla iliyofanyika leo ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.
Dk.Habiba Hassan Omar akila kiapo mbele ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) kuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais,Kazi,Uchumi na Uwekezaji katika hafla iliyofanyika leo ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi akimuapisha Dk.Habiba Hassan Omar kuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais,Kazi,Uchumi na Uwekezaji katika hafla iliyofanyika leo ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.
Mikidadi Mbarouk Mzee akila kiapo mbele ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) kuwa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ katika hafla iliyofanyika leo ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi akimuapisha Nd,Mikidadi Mbarouk Mzee kuwa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ katika hafla iliyofanyika leo ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar
Aboud Hassan Mwinyi akila kiapo mbele ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) kuwa Naibu Katibu Mkuu,Ofisi ya Rais,Fedha na Mipango, Anayeshuhulikia(Fedha na Mipango),katika hafla iliyofanyika leo ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi akimuapisha Nd,Aboud Hassan Mwinyi kuwa Naibu Katibu Mkuu,Ofisi ya Rais,Fedha na Mipango, Anayeshuhulikia(Fedha na Mipango),katika hafla iliyofanyika leo ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.
Viongozi wakuu wa Vikosi vya Ulinzi na Usalama wakiwa katika hafla ya kuapishwa Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu Wakuu,walioapishwa leo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.
Baadhi ya Viongozi mbali mbali waliohudhuria katika hafla ya kuapishwa Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu Wakuu,walioapishwa leo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar. (Picha zote na Ikulu).

Miongoni  mwa waliohudhuria katika hafla hiyo ni pamoja na Makamu wa Kwanza wa Rais, Othman Masoud Othman, Makamu wa Pili wa Rais Hemed Suleiman Abdalla, Jaji Mkuu wa Zanzibar, Omar Othman Makungu na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi, Mhandisi Zena Ahmeid Said.

Wengine ni Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Dkt. Mwinyi Said Haji, Mufti wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kaab, Mkuu wa Mkoa Mjini Magharibi, Kitwana Idrisa Mustafa, mawaziri, wakuu wa vikosi vya ulinzi na usalama pamoja na wanafamilia.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news