TMDA yachukua tahadhari dawa iliyoua watoto 66 nchini Gambia

NA DIRAMAKINI

MAMLAKA ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA), imesema itaendelea kuchukua tahadhari zote kupitia mifumo yake ya udhibiti, ili kubaini endapo dawa inayosadikiwa kusababisha vifo vya watoto 66 nchini Gambia zitafika nchini.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo, Adam Fimbo leo katika taarifa yake kwa waandishi wa habari, amesema dawa hizo hazijawahi kusajiliwa nchini.

Dawa hizo za Promethazine oral solution, Kofexmalin Baby Cough Syrup, Makoff Baby Syrup na Margrip N Cold Syrup zinatengenezwa na kiwanda chenye jina la Maiden Pharmceutical Limited, iliyopo India zilipimwa na kukutwa na viambata vya sumu.

Fimbo amesema dawa hizo zimeonekana kuwa na viambata vinavyosababisha madhara ya kiafya, ikiwa ni pamoja na vifo kwa watumiaji hasa watoto.

“Dawa hizo zimepimwa na kukutwa na viambata vinavyojulikana kama diethlene glycol na ethylene glycol, ambavyo husababisha madhara na hata vifo kwa watumiaji.

“TMDA inapenda kuutarifu umma kuwa dawa hizo zote hazipo katika soko la nchi yetu na hazijawahi kusajiliwa, ili kutumika hapa nchini,” amesema.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news