SIMULIZI YA KUTISHA KATIKA MAISHA-26

NA WILLIAM BOMBOM

Ilipoishia...kila mmoja alikuwa na lake la kusema, wapo waliosema kuwa mtoto huyo kachukuliwa na malaika. Wengine walisema mtoto huyo alikuwa na nguvu kuu kuliko zote, hivyo alikuwa ni nabii wa kweli kutoka kwa mungu.

Endelea

Serikali ilipata misaada mbalimbali toka nje kwa wahisani. Misaada hiyo ilikuwa ya kibinadamu iliyokuwa imelenga kusaidia matatizo ndani ya jamii.

Kikubwa zaidi misaada hiyo ilielekezwa Mkoa wa Mwanza kweye wilaya tatu, yaani Wilaya ya Magu,Nyamagana na Ilemela.

Wafadhili toka Ulaya walimwaga fedha zao kwa serikali, mithili ya mchanga wa bahari ya hindi. Fedha hizo zilikwenda kwenye kada mbalimbali, walijenga kiwanda kidogo cha kutengeneza viatu, mabegi na mikanda eneo la mji wa Igoma uliopo karibu na mji wa Kanyama.

Kiwanda hicho kilijengwa mtaa wa Miti ya Nyerere karibu na kiwanda cha Nzegenuka mkabala wa makaburi ya watu waliopata ajali ya Meli ya MV Bukoba.

Kutoka eneo hilo la kiwanda kwenda mji wa Kanyama ni mwendo wa dakika sita kwa gari inayokimbia. Msaada mwingine wa ufadhili uliotolewa na wazungu hao ilikuwa ni kujenga barabara itokayo Kanyama, Busekwa, Kaguha, Nyamadoke mpaka Buswelu ili ikutane na ile iendayo Nyakato na Ilalela mpaka Igombe.

Msaada mwingine wa kufadhili ulitolewa na wazungu, ilikuwa ni kujenga tenki la maji kubwa eneo la mitaa ya Shamaliwa ndani ya mji wa Igoma.

Tenki hilo lilikuwa na uwezo wa kusambaza lita milioni mia tano kwa siku moja, lilikuwa ni tenki kubwa kuliko matenki yote ya mji wa Mwanza.

Kukamilika kwake lilikuwa na uwezo wa kusambaza maji wilaya zote tatu yaani Nyamagana, Ilemela na Magu. Misaada hiyo ya ufadhili ilikuja haraka sana ndani ya mkoa huo, hakuna hata mmoja ndani ya serikali aliyekuwa akijua nyuma ya pazia ya misaada hiyo kulikuwa na nini.

Makampuni na taasisi za kichawi ya nchi za magharibi baada ya kumpoteza wakala wao Padri Samso na wenzake waliamua kukaa na kubuni njia mbadala ya kuhakikisha wanamuua nabii mtoto.

Lengo lao ilikuwa ni kumpoteza nabii mtoto, wao walikuwa wakiamini mapinduzi ya kiimani ambayo yangeletwa na mtoto huyo yalikuwa makubwa.

Kwa namna hiyo angeweza kubadili mawazo ya watu kuhusu manabii wengine, mtoto huyo angeweza kuleta mapinduzi ya kifikra, kiuchumi na kitaaluma katika nchi za Kiafrika.

Hivyo mabepari wa magharibi na wachawi wakubwa kupitia freemasonry na taasisi zao za siri waliungana kutokomeza ndoto za Afrika.

Kwa kuwa mtoto huyo alitabiriwa kwenye vitabu vya kichawi miaka mingi iliyopita, kupitia unabii huo walikuwa wakifahamu mtoto huyo alikuwa na nguvu kuu kuliko nguvu zote.

Njia pekee ya kuzima ndoto hizo ilikuwa ni kumuua, hivyo taasisi na makampuni hayo yaliamua kuja Afrika kutimiza azima yao.

Njia pekee ya kuingia nchini Tanzania ilikuwa ni kufadhili mambo ya kibinadamu, ndani ya mikataba ya misaada hiyo ya kiufadhili kulikuwa na kipengele cha kuwaruhusu wataalamu toka ulaya kusimamia miradi hiyo angalau kwa muda wa miaka mitano. Ndani ya miaka mitano wangekuwa walishafanikiwa malengo yao ya kumuondoa uhai nabii mtoto huyo.

Kwa kuwa serikali ilikuwa na uhitaji wa misaada hiyo, wao walikubali mikataba hiyo iliyokuwa na hila ndani yake. Hawakuwa wakijua nia ovu zilizokuwa nyuma ya wazungu hao, mara nyingi misaada mingi ambayo huletwa na ndugu zetu weupe huwa ina maslahi makubwa kwa upande wao.

Siku zote watu weupe wanatamani kutunyonya watu weusi, kila wanalolifanya ndani ya nchi zetu huwa na faida kubwa kwa upande wao na hasara kwa upande wa mtu mweusi.

Ni vigumu kwa mtu aliyewauza babu zetu kama wanyama kutupenda, ni hawa hawa watu weupe waliowabaka bibi zetu na kuwalawiti mababu zetu.

Ukichunguza kwa makini miradi yote ilielekezwa karibu ya Mji wa Kanyama, hii haikuwa bahati mbaya bali ilikuwa ni mipango imara iliyokuwa imefanyiwa upembuzi makini.

Maeneo hayo ingekuwa rahisi kumpata mtoto THE BOMBOM, sehemu zingine hazikupelekewa misaada hiyo kwa kuwa lengo lao lilikuwa kuwa karibu na mji wa Kanyama.

Kiwanda cha viatu, mikanda na mabegi kilijengwa haraka huwezi amini, katika kiwanda hicho kulitengenezwa nyumba mbalimbali kwa ajili ya kuishi wazungu hao.

Kwa upande mradi wa maji, ujenzi wa tenki ulikwenda kasi mithili ya mkuki wa manju wa kikurya. Watu walikuwa wakiwaombea maisha mema wazungu hao kwa moyo wa kujitolea, waliwaona wazungu hao walikuwa ni wema kwa msaada wa kibinadamu waliokuwa wameutoa.

Kujengwa kwa tanki kubwa kiasi hicho ilikuwa ni neema kwa raia hao, waliamini kuwa tatizo la maji wilaya hizo lilikuwa limepata ufumbuzi.

Taasisi nyingine ya Ulaya inayojulikana kwa jina sms forever, ilikuwa imetoa msaada kwa parokia ya ndofe. Taasisi hii hujishughulisha na masuala ya kiimani, makao yao makuu ni Marekani.

Taasisi hii inajihusisha na ujenzi wa majumba na vyuo wanavyosoma na kukaa watawa wa kike wa dhehebu la Romani.

Pia inasimamia watawa wa kike zaidi ya milioni moja nchi za Kiafrika, hivyo walikuwa wameamua kujenga nyumba ya watawa eneo la ndofe kilometa ishirini kufika mji wa Kanyama.

Ndugu msomaji hapa nieleze kidogo, zipo taasisi nyingi hasa za nje ya nchi zinafanya kazi tofauti na usajili wao. Hufanya mambo ya hovyo ndani ya nchi za Kiafrika muda mwingine zaidi hata ya shetani.

Kwa mfano taasisi hii ya sms forever kwa nje ilionekana kujihusisha na mambo ya mungu, lakini lengo lake halisi halikuwa hilo.

Ilijihusisha na uzalishaji wa wasagaji na mashoga ndani ya Afrika. Kirefu cha sms ni surtan my saviour forever, yaani shetani ni mokozi wangu milele.

Ili kuficha uchafu wao walitumia kifupi cha sms forever ili watu wasiwagundue, taasisi hiyo pia ina uhusiano mkubwa na zile taasisi zilizotoa msaada wa tanki la maji, barabara na kiwanda cha viatu, mikanda na mabegi.

Kwa upande wa mtoto THE BOMBOM baada ya kupotea pale mlimani mbele za makutano, alichukuliwa na kupelekwa kwenye mapango ya mlima Igoma.

Mlima huo upo eneo la makaburi ya Igoma mtaa wa mission karibu na kanisa la Waadventist Wasabato.Eneo hilo lina milima mirefu ya miamba, kwa watu ambao wamefanikiwa kufika eneo hilo watanielewa kwa urahisi.

Ndani ya milima hiyo huwa kuna mapango, mapango hayo hukaliwa na roho za wahenga waliotutangulia miaka nendarudi.

Yule kizee aliyemchukua hakuwa binadamu wa kawaida, alikuwa ni roho ambaye alivaa mwili wa binadamu wakati anashuka pale Mlima Makamelwa.

Roho hizi wengine huziita mizimu kwa upande wa Waafrika, lakini wazungu wao kwa upande wa mtu mweusi huziita shetani ila kwa upande wao huziita roho mtakatifu.

Ni kawaida kwa wazungu kujikweza kwa vitu vyao hata kama vitakuwa vinazidiwa ubora na vitu vya Waafrika. Ndugu msomaji unapaswa kujua kuwa, nadharia ya mungu mmoja ni ya uongo ilianzishwa kwa maslahi ya wagiriki baada ya kuisambaratisha mji mtakatifu wa Mwafrika wa Kemet.

Ndiyo maana Wajainism, Wahindu, Wabudha, Waislam, Wakristo na Wapagani wana Mungu wao. Mungu ni nguvu kuu yenye kuleta uhai kwa viumbe vyote vinavyoonekana na kutonekana, ndiyo maana mungu wa nabii mtoto THE BOMBOM alimleta kuokoa kizazi kilichokuwa kikinyanyaswa na kunyonywa na watu weupe.

Kazi kuu ya mizimu ni kuwakilisha maombi ya binadamu kwa mungu, kwa kuwa mizimu ni roho tayari walikuwa wakijua mipango ovu iliyokuwa ikipangwa na taasisi za watu weupe dhidi ya mtoto huyo.

Pangoni humo kulikuwa na roho nyingi zilizokuwa zikifanya maombi yao dhidi ya mtoto. Roho hizo zilimuomba mungu kumpa nguvu za ziada mtoto huyo ili aweze kufanikisha mpango wake duniani.

Mambo mengi alifanyiwa mtoto huyo na roho hizo, baada ya hapo walimchukua na kumpeleka kwenye kambi ya kichawi ya Ihush.

Muda huo ilikuwa ni majira ya saa saba usiku, pale kambini aliwakuta wachawi wakimsubilia. Maana wachawi wa Kikongomani waliokuwa naye pale Mlima Makamelwa tayari walikuwa wameshafika kambini hapo.

Kambi nzima ilifurahia kumuona mtoto huyo kafika kambini hapo, ni siku mbili alikuwa hajarudi kambini hao hivyo watu walimkumbuka.

Alipofika alizungumza nao kwa kirefu juu ya shughuli aliyokuwa kaifanya siku mbili hizo. Lakini pia aliwaelezea juu ya taasisi za kichawi za kizungu zilizotuma watu wake maeneo ya Igoma, aliwaeleza kwa kirefu malengo yao maovu dhidi ya kambi hiyo ya kichawi na mtoto THE BOMBOM.

Wachawi kwa pamoja walikubaliana kumtembelea maeneo usiku huo, waliteuliwa wachawi ishirini viongozi wa kambi hiyo na kuelekea maeneo hayo.

Miongoni mwa watu waliotumwa maeneo hayo alikuwa ni mtoto huyo, waliondoka kwa usafiri wa kukata.Hii ni aina ya usafiri ambayo hutumiwa na wachawi wakubwa, ni vigumu sana kwa wachawi wadogo wadogo kumiliki usafiri huu.

Yamkini katika nchi za Afrika unaweza kuukuta kwenye kambi za kichawi mbili au tatu tu, kwa upande wa ulaya hakuna kambi hata moja wanaomiliki.

Usafiri huu huwa inamwagwa dawa fulani chini, hapo huandikwa majina ya eneo unalotoka na unalokwenda. Baada ya hapo wanaosafiri husimama kwenye jina la sehemu wanayotoka, kisha kiongozi wao hukata mchanga wa eneo waliloliandika wanakwenda kwa kutumia jembe maalumu.

Kitendo cha kukata mchanga huo kuuvutia eneo mlilosimama, watu hao hujikuta wamefika eneo wanakwenda. Usafiri huo unaweza kutumia sekunde chache kufika sehemu yoyote ya dunia.

Kwa maana huwa ni kufumba na kufumbua unakuwa umefika eneo unakokwenda, masharti yake ni lazima ufumbe macho kama wewe siye dereva.

Walipanda kwenye usafiri huo wakaianza safari kuelekea kwenye jengo la watawa, ndani ya sekunde nne walikuwa wameshafika eneo la ndofe palipokuwa panajengwa chuo cha watawa.

Walishangaa kuwakuta watu kibao wakiendelea na shughuli zao, watu hao walikuwa ni wachawi wa Kizungu, walikuwa wanazindika eneo hilo huku wakiwa wamewabeba Waafrika watatu mateka.

Mateka hao walikuwa wa kiume na kike, mzungu mmoja aliyeonekana kuwa kiongozi wa wachawi hao mkononi alikuwa kashika jambia.

Alimsogelea mateka mmoja kisha akamwekea jambia hilo shingoni mwake, bila huruma alianza kumchinja mateka huyo wa Kiafrika.

Damu zikasambaa eneo hilo mfano wa mvua za rasharasha, yule mateka aliyechinjwa aliachiwa akawa anarukaruka mithili ya kuku aliyechinjwa.

Wakati huo wachawi wote wa Kizungu wakawa wanazungumza kwa pamoja, We need divine power!!We need divine Power!!.

Yule mateka alidondoka chini na kutulia, hakuwa na uwezo wa kufanya jambo lolote. Kichwa chake kilikuwa kimetenganishwa na kiwiliwili kwa jambia la mzungu huyo, mambo hayo yalikuwa yakifanyika mbele ya macho ya kundi la mtoto THE BOMBOM.

Wale wazungu wachawi hawakuwa na uwezo wa kuwaona kundi la mtoto THE BOMBOM. Ikafika zamu ya mateka wa kike, walimvua nguo zake kisha wakaanza kumuingilia kinyume cha maumbile.

Masikini mama wa Kiafrika alikuwa akiteseka ndani ya nchi na bara lake. Wazungu walikuwa wakimfanyia vitu vya hovyo, kitendo hicho kilimuudhi mtoto THE BOMBOM akataka kumsaidia mwanamke huyo toka kwenye mikono ya wapuuzi hao.

Mtoto huyo alianza kumsogelea mzungu huyo aliyekuwa akimuungilia kinyume mama huyo wa Kiafrika, Mkuu wa kambi ya Ihushi alilitambua nia ya mtoto huyo.

Alimzuia kwa ishara mtoto huyo akatii, waliendelea kumlawiti mama huyo wakipokezana kwa zamu. Kwa kuwa walikuwa wazungu kama ishirini wote wa kiume waliendelea kumuingilia mpaka mama huyo alipozirai, walimmalizia kwa kumkata kichwa kwa jambia kisha walimzika kwenye msingi wa majengo ya chuo cha watawa hao.
Hali haikuwa nzuri hata kidogo maeneo hayo, wachawi hao waliendelea kuzindika eneo hilo. Punde si punde walionekana wachawi wawili wakija maeneo hayo, walikuwa wamebeba kiroba kilichokuwa kinachezacheza.

Walipofika maeneo hayo walikishusha kiroba hicho na kukifungua, kwa ndani walikuwa wamebeba mtu mwenye ulemavu wa ngozi yaani albino.

Walimbwaga chini mithili ya pakacha kisha wakaondoka, baada ya dakika tatu walirudi tena wakiwa na kiroba kingine. Walikifungua kiroba hicho kilichokuwa na binadamu mwenye ulemavu wa miguu yaani kiwete. Watu hao walipaswa kuchinjwa ili kuleta upatanisho baina ya Mungu wa wazungu hao pamoja nao.

Ndugu msomaji mambo yanazidi kusonga mbele, wazungu wameanza kutoa kafara ili kuzindika majengo yao kabla ya kuanza kumshughulikia mtoto THE BOMBOM.

Unadhani mtoto huyo atakubaliana na unyama huo unaofanywa na watu hao mbele yake? Endelea kufuatilia kisa hiki cha kusisimua sehemu inayofuata.

MIDIMU NKOI

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news