BREAKING News: Kocha wa Taifa Stars awatimua Kapombe na Nyoni

NA MWANDISHI DIRAMAKINI

Kocha wa Taifa, Kim Poulsen amewatimua katika timu ya Taifa walinzi wawili wa timu hiyo Shomar Kapombe na Erasto Nyoni.
Vijana hao wanadaiwa kuchelewa kuingia kambini, jambo ambalo halikubaliki.

Kwa mujibu wa taarifa zilizoifikia DIRAMAKINI Blog muda huu, muda alioweka kocha huyo kwa wachezaji hao ambao waliwasili leo mchana wakitokea Morocco ulikuwa ni saa kumi na moja jioni.

Aidha,taarifa kutoka kambi ya Stars usiku huu wachezaji hao hawajaripoti na kocha huyo hana taarifa yeyote,hivyo ameagiza wakiripoti wasipokelewe katika kile alichosema kujenga nidhamu ya timu hiyo ili kusonga mbele.

Taarifa zaidi fuatilia hapa..

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news