Wapinzani wamtaka Askofu Gwajima arudi shule, Zitto, Mchungaji Msigwa wamsuta kwa kauli zake

Pengine huenda sasa, Watanzania wengi wameanza kuchoshwa na kile wanachodai ni mipasho ya Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kawe, Josephat Gwajima kwa kuendelea kutumia madhabau takatifu kulumbana na mamlaka za Serikali hususani kuhusiana na chanjo dhidi ya janga la UVIKO-19.

MWANDISHI DIRAMAKINI anakusogezea kwa karibu chambuzi zilizotolewa huku zikiwa na maonyo kwa Askofu Gwajima kutoka kwa mchambuzi wa masuala ya kisiasa, Thadei Ole Mushi huku Mheshimiwa Zitto Kabwe na Mchungaji Peter Msigwa wakichambua kupitia video fupi chini.

Ndugu Thadei Ole Mushi anamtaka Askofu Gwajima kutambua kuwa, Waziri wa Afya, Mheshimiwa Dkt. Dorothy Gwajima anatumikia kiapo  mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, hivyo asidhalilishwe.

"Dkt.Dorothy yeye anatekeleza majukumu ya Kiserikali kwa mujibu wa Sheria.Hata kama aliwahi kukosea huko nyuma akarudi kurekebisha makosa yake sioni tatizo. Waziri yeye alikula kiapo cha kumtii Rais na ndicho anachokitumikia kwa uaminifu.Sasa yeyote anayemlaumu huyo hakumbuki hiki kiapo kabisa,"anafafanua Ole Mushi.

Mchungaji Peter Msigwa anafunguka

"Kwa jicho la nyama unaweza kufikiri Askofu Gwajima anapambana na Dorothy Gwajima yeye binafsi. Lakini kwa jicho la kitafiti ni kuwa Askofu Gwajima anamtumia Dorothy Gwajima kuipiga mamlaka teuzi. Hapa haihitaji Rocket science kuling'amua,"anaongeza Ole Mushi.


Zitto Kabwe afunguka

"Kwa bahati mbaya sana Waziri Gwajima ni kama vile  wenzake, kwa maana ya mhimili wa dola wamemwachia sekeseke hilo la chanjo peke yake. Hii issue ni ya kitaifa na imebeba usalama wa nchi lakini, the way inavyojadiliwa inataka kufanywa kuwa ni issue ya kifamilia. Na leo waziri kwa kuwa anatumikia kiapo chake kadhalilishwa kabila lake la Kinyiramba,"anafafanua Ole Mushi.

Tayari Askofu Gwajima pamoja na Mbunge wa Ukonga (CCM) Jerry Silaa wameitwa mbele ya Kamati ya Maadili na Madaraka ya Bunge ili kujibu tuhuma mbalimbali ikiwemo kusema uongo na kushusha hadhi na heshima ya Bunge.

Taarifa iliyotolewa Jumamosi Agosti 21, 2021 na Kitengo cha Mawasiliano Ofisi ya Bunge, imeeleza wabunge hao wameitwa mbele ya Kamati hiyo kwa agizo la Spika wa Bunge Job Ndugai.

Leo Askofu Gwajima ataanza kuhojiwa na kesho atafuatiwa na Jerry Silaa.Nini hatima yao. Endelea kufuatilia DIRAMAKINI Blog tutakujuza yote.

Kubwa zaidi tuendelee kuchukua tahadhari dhidi ya janga la UVIKO-19 na kila mmoja wetu afike vituo mbalimbali vilivyopo nchini kupata chanjo. 


MUHIMU

UNATAMANI DIRAMAKINI BLOG TUWE HEWANI SAA 24 KUKUPA HABARI ZA KINA KILA DAKIKA, TUNAOMBA UTUUNGE MKONO KWA KUCHANGIA GHARAMA ZA MAWASILIANO NA INTANETI KWA WAANDISHI WETU POPOTE WALIPO NDANI NA NJE YA TANZANIA; TUNAPOKEA MCHANGO WAKO KUPITIA 0719254464 (Tigo Pesa-Godfrey Nnko) AU UKIHITAJI NAMBA YA BENKI TUJULISHE. MUNGU AKUBARIKI SANA KWA SAPOTI YAKO. ASANTE

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news