TUVUNE MAJI YA MVUA

NA MOHAMED OMARY MAGUO

UTENZI wa elimu na hamasa ya utunzaji wa mazingira na uhifadhi wa maji katika kipindi hiki cha mvua;

1


Mikoa mingi yanyesha


Na maji kutiririsha


Tuvune yasijeisha


Tutumie kiangaziUvunaji wa maji ya mvua unaweza kumsaidia mkulima kuboresha kilimo chake na kujiongezea kipato zikiwemo faida nyingi katika maisha ya kila siku ya binadamu. (Picha na Mtandao).

2


Mapaa yetu safisha


Na gata kuzitayarisha


Mvua inaponyesha


Maji safi kisimani


3


Mabwawa kutegesha


Ili maji kukingisha


Tusiyaache yake'sha


Makorongo kubakisha



4


Mkondo kutopindisha


Mito kuinawirisha


Kwa maji kuijazisha


Huo ndio uzalendo



5


Sijaribu kuchepusha


Mvua inaponyesha


Bali wewe yavunisha


Maji yanayopotea



6


Mmomonyoko komesha


Ardhi kuistawisha


Tuvune inaponyesha


Yatufae Kiangazi



MTUNZI


Dkt. Mohamed Omary Maguo


Mshairi wa Kisasa


Mhadhiri na Mkurugenzi wa Mawasiliano na Masoko Chuo Kikuu Huria cha Tanzania

25/2/2022

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news