Meneja wa kampasi ya Dodoma ya Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA), Prof. Epaphra Manamba amesema katika kuendana na mahitaji ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 IAA itaendelea kuwekeza katika mitaala itakayojikita kwenye elimu – ujuzi (Competence based ) na ubunifu ili kuwaandaa wataalam watakaokuwa na uwajibikaji jumuishi katika kujenga Uchumi Jumuishi.

Prof. Manamba ameyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika banda la IAA kwenye Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma.
“Dira ya Taifa ya 2050 imeipa sekta binafsi nafasi kubwa, tunapoongelea uwajibikaji jumuishi na uchumi jumuishi sekta binafsi inahusika kwa asilimia 100;sekta binafsi imepewa nguvu kwa sababu maendeleo ya nchi hii yatachangiwa na sekta binafsi na serikali itaandaa miundombinu ili kuiwezesha sekta binafsi kufanya kazi yake.”
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo
















