Jichunguze mwenyewe, unabii na utimilifu wa Agano la Kale na Jipya unathibitisha-Lee

NA DIRAMAKINI

MWENYEKITI Man-hee Lee wa Kanisa la Shincheonji la Yesu, Hekalu la Hema ya Ushuhuda (Shincheonji Church of Jesus) amelieleza kusanyiko kubwa la wachungaji kupitia semina ya mtandaoni kuwa,kitabu cha Ufunuo katika Biblia Takatifu ni chakula cha milele na kila mmoja anapaswa kulifanya neno na maombi kuwa sehemu ya maisha yake.

“Kitabu cha Ufunuo ni chakula cha milele kwa ajili yetu sisi kula.Chakula cha shetani ni divai ya uzinzi katika Ufunuo 17 na 18, na hili ni tunda la mema na mabaya. Je? Haikuandikwa kwamba Ulimwengu wote umeanguka kwa sababu ya divai ya uzinzi?;
Ameyasema hayo hivi karibuni kupitia kusanyiko hilo ambalo liliwakutanisha watumishi wa Mungu kutoka pande mbalimbali za Dunia kupitia hadhara ya Biblia Mtandaoni kuhusu yaliyomo kwa jumla katika Biblia.

Akishuhudia neno baada ya siku 20 mfululizo wa kufafanua unabii na uhalisia uliotimizwa wa sura zote za Kitabu cha Ufunuo aliwataka wachungaji kufanya maamuzi sahihi.

Lee alisisitiza kwamba, unabii wa kitabu cha Ufunuo ulitimizwa na kutimia, na akaomba kwa mara nyingine tena kuthibitisha hilo kupitia ushuhuda wa shahidi aliyeuona pale yalipotimia.

Alishuhudia uhalisia kwa kutafsiri kitabu kizima cha Ufunuo sura baada ya sura kupitia semina hiyo ya hadhara yenye kichwa ‘Unabii na Utimilifu wa Agano la Kale na Jipya’ iliyofanyika kwenye chaneli rasmi ya YouTube ya Shincheonji Church of Jesus.
Mwenyekiti Lee, ambaye alifanya mhadhara mnamo Julai 4, mwaka huu ambao ulifanya muhtasari wa semina za kozi za msingi, za kati na za juu, ambazo Kanisa la Shincheonji limekuwa likifungua tangu mwaka jana, alifanya semina ya hadhara baada ya siku 20 akiuliza tena kuthibitisha ukweli wa Kitabu cha Ufunuo.

Kama mfululizo wa semina za mtandaoni zilizofanywa na Shincheonji Church of Jesus hivi karibuni watazamaji milioni 20 wameongezeka, na maombi ya nyenzo za kufundishia neno yameongezeka sio tu nje ya nchi lakini pia ndani, hali hii inaonesha shauku inayokua katika ushuhuda wa kweli wa Kanisa la Shincheonji la Yesu.

Kanisa la Shincheonji la Yesu lilirekodi ongezeko la kila mwaka la zaidi ya washiriki 20,000 mnamo mwaka 2020 na 2021, hata wakati UVIKO-19 ikiwa imeshika kasi.

Aidha,katika nusu ya kwanza ya mwaka huu pekee, zaidi ya watu 100,000 walichukua masomo ya mtandaoni, na kufanya Sherehe ya Kuhitimu ya Watu 100,000 kuelekea mwishoni mwa mwaka huu.

Licha ya kukashifiwa na kuteswa na madhehebu yaliyopo na baadhi ya makundi ya kisiasa, inatathminiwa kuwa ongezeko hilo la haraka la idadi ya wanachama ni kutokana na ushuhuda wa neno kupitia semina mbalimbali za hadhara.

Kwa hivyo, Kanisa la Shincheonji la Yesu linapanga kutoa fursa zaidi za kuangalia moja kwa moja ushuhuda wa ukweli kwamba unabii wa Biblia umetimizwa.

Wakati huo huo, Mwenyekiti Lee alielezea usaliti wa watu waliochaguliwa, ambao walifanya agano na Mungu, kuanzia kwa Adamu, kupitia kwa Nuhu na Ibrahimu, na hadi ujio wa kwanza wa Yesu, na mchakato wa kuanzisha Agano Jipya katika Ujio wa Pili wa Yesu.

Mwenyekiti Lee, alisema kwamba Mathayo 24, ambayo ilitabiri wakati wa Ujio wa Pili wa Bwana, na kitabu kizima cha Ufunuo, lazima pia kutimizwa ili kuamini katika Biblia, alitoa ushuhuda wa kina kuhusu uhalisia wa utimizo huo.

“Mtu huyu haongei nilichojifunza kutoka kwa mtu yeyote, wala siongelei nilichojifunza kupitia utafiti. Ninasema ninachokiona kwa macho yangu na kile ninachosikia kwa masikio yangu,”alisema.

Mwenyekiti Lee ambaye alishuhudia matukio yakitendeka sura baada ya sura kutoka Ufunuo 1, alieleza hilo pale ufalme wa Mungu utakaposimamishwa, Mungu anaweza kuja hapa duniani.

Pia alisisitiza umuhimu wa kujiunga kwa watu 144,000 walioumbwa upya baada ya kutiwa muhuri na neno la Mungu na umati mkubwa waliovaa mavazi meupe kutoka katika ile dhiki kuu, na kueleza mwendo wa wokovu wa Mungu katika kitabu cha Ufunuo.

“Wachungaji walio na matumaini Mbinguni, lazima wafanye uamuzi sahihi.Tunaweza kujifunza uhalisia wa Ufunuo kwa kusikia kutoka kwa mtu aliyeshuhudia mambo hayo pale yalipotokea baada ya kupokea kitabu kilichofunguliwa kulingana na Biblia, kulingana na mapenzi ya Mungu. Kitabu cha Ufunuo ni chakula cha milele kwa ajili yetu sisi kula.Chakula cha Shetani ni divai ya uzinzi katika Ufunuo 17 na 18, na hili ni tunda la mema na mabaya.

"Je, haikuandikwa kwamba ulimwengu wote umeanguka kwa sababu ya divai ya uzinzi?.Mtu huyu amejionea na amesikia mwenyewe. Ndiyo maana hata ninajua nyuso na majina ya wasaliti katika kitabu cha Ufunuo. Hata nikifa nikishuhudia, hairuhusiwi kusema sitahubiri neno la Mungu tena,”alisema.

Katika hatua nyingine, Kanisa la Shincheonji Church of Jesus lilifanya semina kwa kuanzia na mihadhara juu ya sura zote za kitabu cha Ufunuo mnamo Oktoba mwaka jana, 'Ushuhuda wa Mifano ya Siri za Ufalme wa Mbinguni na Ukweli', na 'Ushuhuda wa Ufunuo kwa Sura katika Agano la Kale na Jipya' ambalo limefanyika hadi mwanzoni mwa mwezi huu. Semina inaweza kutazamwa kwenye chaneli rasmi ya YouTube ya Shincheonji Church of Jesus.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news