Afisa Mtendaji Mkuu BRELA,Godfrey Nyaisa atunukiwa tuzo ya utendaji bora nchini

NA MWANDISHI WETU

AFISA Mtendaji Mkuu kutoka Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Bw. Godfrey Nyaisa amepata tuzo ya utendaji bora na kuwa miongoni mwa Watendaji Wakuu Bora 100 waliotunukiwa tuzo hizo kwa mwaka 2022.
Tuzo hiyo imetolewa Novemba 27, 2022 katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam, ambapo Mkurugenzi wa Leseni kutoka BRELA Bw. Andrew Mkapa aliipokea kwa niaba yake. Mgeni rasmi katika hafla hiyo alikuwa ni Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda wa Zanzibar Mhe. Omar S. Shaaban (Mb).
Bw. Nyaisa ni miongoni mwa Wakurugenzi Wakuu na Maafisa Watendaji Wakuu sita bora wa Taasisi za Serikali ambao wamepata tuzo, akiwemo pia Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (PSSSF) Bw. Hosea Kashimba, Mkurugenzi Mtendaji wa STAMICO, Dkt. Venance Mwasse, Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa, Dkt. Noel Lwoga, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege Tanzania, Bw. Ladislaus Matindi na Afisa Mtendaji Mkuu wa kutoka Watumishi Housing Investment, Dkt. Fred Msemwa.
Akizungumza na watumishi wa BRELA katika Ofisi za BRELA leo tarehe 28 Novemba, 2022 baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo Bw. Nyaisa amesema ushirikiano anaoupata kutoka kwa watumishi katika utekelezaji wa majukumu ya kila siku ndiyo uliowezesha kutambuliwa na kuwa miongoni mwa Maafisa Watendaji Wakuu waliopata tuzo.
Bw. Nyaisa amesema tuzo hiyo iwe chachu ya utendaji bora wa kazi kwa watumishi wote kwani utendaji mzuri wa kazi unaofanywa na watumishi ndiyo uliyoiwezesha BRELA kutambulika na kuchaguliwa miongoni mwa Taasisi za Serikali.
Hafla hiyo inayojulikana kama Tanzania Top 100 Executive Awards ambapo kwa mwaka 2022 ni mara ya pili kufanyika, imeandaliwa na Kampuni ya Easternstar kwa kushirikiana na KPMG Tanzania na imehudhuriwa na washiriki zaidi ya 300 kutoka Taasisi za Serikali na Sekta Binafsi za Tanzania Bara na Visiwani.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news