Wizara ya Ardhi yatoa siku 30 kwa wadaiwa kodi ya pango la ardhi

NA DIRAMAKINI

WIZARA ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imewajulisha wananchi kuwa kwa mujibu wa Sheria ya Ardhi (SURA ya 113) kifungu cha 44 kila mmiliki wa ardhi anatakiwa kutimiza masharti ya umiliki ikiwa ni pamoja na sharti la kulipa kodi ya pango la ardhi kila mwaka.
Hayo yamebainishwa kupitia taarifa iliyotolewa Novemba 18, 2022 na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dkt.Allan Kijazi.

Pia ameeleza kuwa, baadhi ya wamiliki wamevunja sharti hilo kwa mujibu wa kifungu cha 45 la kulipa kodi ya pango la ardhi kila mwaka.

"Hivyo, natoa taarifa kwamba, wananchi wote wanaodaiwa kodi ya pango la ardhi wanapewa nafasi ya mwisho kulipa kodi ya pango ndani ya siku 30 kuanzia tarehe ya tangazo hili (Novemba 18, 2022). Baada ya muda huu kupita taratibu za kisheria za ubatilisho wa miliki zitaendelea,"amefafanua Dkt.Kijazi kupitia taarifa hiyo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news