Piga mpira sio mwanamke

DAR ES SALAAM-Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma ametoa rai kwa Vilabu vya Mpira wa Miguu nchini kuunga mkono juhudi za kupinga ukatili kwa wanawake na watoto wa jinsia zoteili kukomesha na kumaliza vitendo hivyo kwenye jamii.
Mhe. Mwinjuma ametoa rai hiyo Oktoba 18, 2023 wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto wa jinsia zotekupitia mchezo wa mpira wa miguu ijulikanayo kama "Piga Mpira sio Mwanamke"

Amesema ni wakati muafaka kwa vijana wa kiume, akina baba kujadili tatizo hilo ili kuwarithisha watoto Taifa lenye utulivu, amani, upendo na Maendeleo huku akibainisha kuwa kampeni hiyo ambayo iko chini ya Taasisi ya Thamani Women Tanzania ikiongozwa na Mkurugenzi wake Nafue Nyange mpaka sasa imeungwa mkono na Vilabu vya Simba SC, Azam FC na Singida Fountain Gate.

"Mchezo wa mpira wa miguu umesaida kuunganisha watu na jamii. Jambo hili linaufanya mpira uwe zaidi ya mchezo na zana muhimu ya kuvunja vizuizi vya kijamii na kiutamaduni nje ya uwanja. Wachezaji kutoka nyanja mbalimbali wana jukumu la kufanya kazi pamoja kufikia lengo moja la ushindi dhidi ya timu pinzani.

"Leo tunashuhudia vilabu hivi vitatu vikiungana dhidi ya mpinzani mmoja Ukatili,"amesisitiza Mhe. Hamis Mwinjuma.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news