Kagera Sugar yampa talaka Kocha Meck Mexime

KAGERA-Uongozi wa Klabu ya Kagera Sugar ya mkoani Kagera umefikia uamuzi wa kumfuta kazi Kocha Meck Mexime.
Uamuzi huo unakuja ikiwa ni siku moja tu baada ya kupokea kichapo cha mabao 4-0 kutoka kwa Azam FC mchuano wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara.

Uamuzi huo umefikiwa baada ya Kagera Sugar kuwa na mwendo wa kusuasua kwenye michuano ya Ligi Kuu ya NBC Tanzania ikiwa wameshuka dimbani mara 13 na kukusanya alama 13 tu.

Mexime alijiunga na Kagera Sugar katikati ya msimu uliopita kuchukuwa nafasi ya Kocha raia wa Kenya, Francis Baraza.

Mbali na Mexime, pia Kagera Sugar wametangaza kuachana na Kocha wao wa viungo, Francis Mkanula.

"Tumefikia maamuzi ya kuachana na Kocha Mkuu, Mecky Mexime, vile vile tumeachana na Kocha wa Viungo Francis Mkanula."
Kwa mujibu wa Kagera kikosi cha timu hiyo kitakuwa chini ya Kocha wa mpito, Marwa Chamberi ambaye ataongoza timu wakati zoezi la kusaka kocha mpya likiendelea.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news