Rais Dkt.Mwinyi amtunuku nishani ya heshima (order of praise) Rais Dkt.Samia


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akivalishwa Nishani ya Mapinduzi ya Viongozi wenye sifa za Kipekee (Order of Praise) na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi kwenye hafla iliyofanyika katika viwanja vya Ikulu ya Zanzibar tarehe 11 Januari, 2024. Rais Samia ametunukiwa Nishani hiyo katika kuadhimisha miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipongezwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi mara baada ya kutunukiwa Nishani ya Mapinduzi ya Viongozi wenye sifa za Kipekee (Order of Praise) katika kuadhimisha miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964 kwenye hafla iliyofanyika katika viwanja vya Ikulu ya Zanzibar tarehe 11 Januari, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye hafla ya Utoaji wa Nishani iliyofanyika kwenye viwanja vya Ikulu ya Zanzibar tarehe 11 Januari, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akifurahia jambo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi wakati wa hafla ya utoaji wa Nishani ya Mapinduzi ya Viongozi wenye sifa za Kipekee (Order of Praise) katika viwanja vya Ikulu ya Zanzibar tarehe 11 Januari, 2024.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news