Mafuriko mto Miombo Kilosa yazoa daraja

MOROGORO-Mkuu wa Wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro,Shaka Hamdu Shaka amelazimika kutembea zaidi ya kilomita tano ndani ya maji.

Ni wakati wakiwa katika harakati za kusaidia kuokoa wananchi waliopata mafuriko kufuatia kujaa mto Miombo baada kupokea maji mengi kutoka milimani.
Awali Mkuu wa Wilaya na Wajumbe wa Kamati ya Usalama walifika eneo ambalo daraja linalounganisha vijiji vitatu katika Kata ya Nyameni Zombo ambalo limechukuliwa na maji na kusababisha huduma za usafiri na usafirishaji kusimama.
Hata hivyo, wakati wakitoka eneo hilo wakajikuta wamezungukwa na maji na kulazimika kuanza kutembea kujinusuru sambamba na kuwasaidia wananchi wengine ambao bado walikuwa katika makazi yao.
Mafuriko hayo yaliyosabibishwa na mvua kubwa zilizonyesha milimani,hakuna athari za kibinadamu zilizotokea zaidi ya kuharibu miundombinu ya madaraja, barabara na makazi ya wananchi ambapo zaidi ya kaya 120 zimeingiliwa na maji.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news