Serikali yatenga shilingi bilioni 2.6 kugharamia taulo za kike shuleni

DODOMA-Naibu Waziri Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe Zainab Katimba amesema, katika mwaka wa fedha 2023/24 Serikali ilitenga Shilingi Bilioni 2.64 kwa ajili ya kugharamia taulo za kike ambapo kati ya fedha hizo Shilingi bilioni 1.06 ni za ruzuku ya uendeshaji na Shilingi bilioni 1.58 ni fedha kutoka mapato ya ndani ya halmashauri.
Mheshimiwa Katimba ameyasema hayo bungeni leo wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Mheshimiwa Nora Mzeru aliyehoji nini mpango wa serikali kutenga bajeti kwa ajili ya taulo za kike mashuleni.

Amesema, hadi kufikia Machi, 2024 shilingi Bilioni 2.2 zimetumika ambapo pia wadau mbalimbali walichangia jumla ya Sh bilioni 1.5 na miradi ya shule ya elimu ya kujitegemea ilichangia shilingi milioni 119.5.

Mheshimiwa Katimba amezisisitiza halmashauri zote nchini kutenga bajeti kwa ajili ya upatikanaji wa taulo za kike shuleni.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news