DODOMA-Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Aprili 27, 2025 ni mgeni rasmi katika Mdahalo wa upatikanaji Mitaji ya Fedha na Fursa za Maendeleo ya Ushirika, mdahalo huo unafanyika katika ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma.
Awali wakati akitembelea mabanda ya maonesho, Mheshimiwa Majaliwa alizindua mradi wa kwanza wa utekelezaji wa Programu ya BBT (BBT PROJECT 1). Pia alizindua ramani ya Shoroba za Kilimo nchini.
Tags
Benki ya Ushirika Tanzania
Habari
Ofisi ya Waziri Mkuu
Vyama vya Ushirika Tanzania
Wizara ya Kilimo Tanzania







