Kongamano la Kiswahili lafana Namibia

WINDHOEK-Ubalozi wa Tanzania nchini Namibia kwa kushirikiana na Chuo cha Triumphant ziliandaa Kongamano la Kwanza la Kiswahili lililozungumzia mchango wa lugha ya Kiswahili katika harakati za ukombozi wa nchi za Kusini mwa Afrika hususan Namibia.
Mgeni Rasmi katika Kongamano hilo lililofanyika Aprili 25, 2025 alikuwa Mheshimiwa Lt.Gen.(Rtd) Epaphras Denga Ndaitwah, Mwenza wa Mheshimiwa Rais wa Namibia.
Mtoa mada Mkuu kutoka Tanzania alikuwa Bi.Consolata Mushi, Katibu Mtendaji wa BAKITA ambaye alimwakilisha Mhe.Prof.Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi (MB), Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Watoa mada wengine kutoka Tanzania walikuwa Balozi Lt.Gen.(Rtd) Abdulrahman Shimbo, Balozi Brig.Gen.(Rtd) Francis Mndolwa na Dkt .Eliah Victor, Mkurugenzi wa Vipindi kutoka TBC.
Kwa upande wa Namibia,mtoa mada alikuwa ni mmoja wa Wapigania Uhuru wa Namibia aliyeishi Kongwa, Dodoma nchini Tanzania.

Aidha,Kongamano hilo lilihudhuriwa wa Wapigania Uhuru wa Namibia walioishi Tanzania,Vijana wa Namibia waliozaliwa uhamishoni, Mabalozi, Wanazuoni,Wanafunzi pamoja na Waandishi wa Habari.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news