Dkt.Hassan Abbasi akagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya kimkakati Ngorongoro

ARUSHA-Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi leo tarehe 10 Mei, 2025 amefanya ziara katika eneo la Hifadhi ya Ngorongoro na kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya kimkakati ikiwepo mradi wa Ujenzi wa Jengo la kisasa la Makumbusho ya Jiolojia, Ujenzi wa Jengo la Makao makuu ya NCAA linalojengwa nje ya Hifadhi ya Ngorongoro katika Wilaya ya Karatu.
Ujenzi wa Miradi hiyo imefikia zaidi ya asilimia 90 na inatarajiwa kukamilika hivi karibuni.
Dkt. Abbasi amesisitiza Menejimenti ya NCAA ikiongozwa na Kamishna wa Uhifadhi Dkt. Elirehema Doriye kuendelea kusimamia utekelezaji wa Miradi hiyo na kuhakikisha inakamilika kwa wakati, kuzingatia thamani ya fedha na viwango vya kimataifa kwa ajili ya kuhudumia wageni.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news