Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limekifunga kiwanda cha kutengeneza zege cha JUYE Concrete Company Ltd kilichopo Mikocheni, jijini Dar es Salaam, kufuatia tuhuma za uchafuzi wa mazingira unaowaathiri wakazi wa maeneo jirani.
Zuio hilo limetolewa Februari 12, 2026, na Meneja wa Uzingatiaji wa Sheria wa NEMC, Hamadi Taimuru, baada ya kufanya ziara ya kushtukiza kiwandani hapo kukagua utekelezaji wa maagizo yaliyokuwa yametolewa awali.Kwa mujibu wa Taimuru, kiwanda hicho kilianza kukaguliwa tangu mwaka jana na kimepewa maelekezo mara nne ili kurekebisha kasoro zilizobainika. Hata hivyo, malalamiko kutoka kwa wakazi wa karibu kuhusu vumbi na maji taka yameendelea kuripotiwa.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo














