Serikali imeiagiza Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kubuni na kuimarisha njia rahisi za kufikisha matokeo ya tafiti kwa Wizara husika na taasisi nyingine zinazohusika, ili matokeo hayo yafanyiwe kazi na kusaidia kutatua changamoto zinazotokana na mabadiliko ya tabianchi.
Hayo yalibainishwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Daniel Mushi, wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kwanza wa kila mwaka wa maendeleo ya utafiti chini ya Programu ya Utafiti wa Mabadiliko ya Tabianchi.
Profesa Mushi alisema matokeo ya tafiti ni muhimu kwa taifa kwa kuwa yataisaidia Serikali na Wizara husika kupata suluhisho la changamoto mbalimbali, ikiwemo uharibifu wa miundombinu unaosababishwa na mabadiliko ya tabianchi.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo
.jpeg)
.jpeg)
















