KIGOMA-Mkuu wa Kikosi cha Mbwa na Farasi Mkoa wa Kigoma Mkaguzi wa Polisi (INSP) David Kaimukilwa amewataka wanafunzi wa Shule ya Sekondari Katubuka iliyopo Manispaa ya Kigoma Ujiji kuwatumia Mbwa kuimarisha usalama wa mali zao.
Hayo yamesemwa Machi 13,2026 ambapo amewataka wanafunzi hao kufuga Mbwa majumbani mwao kwani Mbwa ni mlinzi hutumika kuimarisha usalama wa mali endapo atafugwa na kuhudumiwa vyema.
Pamoja na hayo amewataka wanafunzi hao kuendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu.



