Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imekutana na wadau kutoka sekta mbalimbali kwa lengo la kujadili namna ya kuboresha ukusanyaji wa mapato pamoja na kuimarisha utendaji kazi wa mamlaka hiyo.
Mkutano huo umefanyika Mei 11, 2026 jijini Dar es Salaam ukilenga kusikiliza kero na changamoto zinazowakabili wadau katika utekelezaji wa majukumu yao ya kikodi, sambamba na kutafuta suluhisho la changamoto hizo kwa pamoja.
Aidha, TRA imeeleza kuwa vikao vya aina hiyo vitaendelea kufanyika kila baada ya miezi mitatu ili kutoa nafasi kwa wadau kuwasilisha maoni yao na kujadili maboresho mbalimbali yanayohusu huduma za kodi nchini.
Akizungumza katika mkutano huo, Kamishna Mkuu wa TRA, Yusuph Mwenda amesema mamlaka hiyo itaendelea kutoa elimu kwa walipakodi, kuboresha mifumo ya utoaji huduma pamoja na kuhakikisha utekelezaji wa maazimio yaliyojadiliwa unaanza mara moja.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo














