SERIKALI ya Sudan Kusini imesema kuwa, imeiomba Benki ya Afrika ya Uingizaji na Usafirishaji Nje Bidhaa (Afreximbank) iipe mkopo nchi hiyo wa kuweza kukabiliana na athari mbaya za virusi vya Corona (Covid-19).
Naibu Waziri wa Kilimo na Usalama wa Chakula nchini humo, Lily Albino Akol amesema, mkopo huo utatumika kuisaidia serikali kufanikisha vipaumbele vyake ikiwa ni pamoja na kupunguza athari mbaya za ugonjwa wa corona katika sekta ya uchumi nchini humo.
Akol ameyabainisha hayo kupitia mahojiano yana redio serikali ya Shirika la Utangazaji la Sudan Kusini (SSBC).
Naibu huyo amesema,wapo katika hatua za mwisho za kufanikisha kutolewa mkopo huo na kurejea kusema kuwa, mkopo huo utatumika kukabiliana na madhara ya kiuchumi yaliyosababishwa na ugonjwa wa COVID-19 katika nchi hiyo.
