Rais mstaafu Lissouba afariki

RAIS wa zamani wa Jamhuri ya Congo Brazzaville, Pascal Lissouba (88) aliyeitawala nchi hiyo kuanzia mwaka 1992 hadi 1997 amefariki dunia akiwa nchini Ufaransa.

Honore Sayi ambaye ni mbunge na Msemaji wa Chama cha Lissouba cha UPADS alichokiunda mwaka 1991 amethibitisha habari hiyo na kuongeza kuwa, Lissouba amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mfupi akiwa nje.

Pia mtoto wake Jeremie Lissouba ambaye ni mwanasheria, naye amethibitisha kifo hicho.

Baada ya kupoteza madaraka mwaka 1997 kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe, rais huyo wa zamani wa Congo Brazzaville alikimbilia Ufaransa mwaka 2004 baada ya kuishi Libreville, Burkina Faso na London kwa muda.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here