Tanzania Distilleries Limited (TDL) yawaongezea tabasamu wakulima wa zabibu

KAMPUNI  ya Tanzania Distilleries Limited (TDL), imeeleza dhamira yake ya kuendeleza kilimo cha zabibu mkoani Dodoma pamoja na matarajio yake ya kuingia mikataba ya kununua zabibu moja kwa moja kutoka kwa wakulima wadogo.

Mchango wa TDL wa sera yake ya kununua malighafi nchini  na dhamira ya kukuza sekta ya kilimo cha zabibu inaenda sambamba na jitihada za  Serikali za kuboresha maisha ya wakulima wadogo na kukuza uchumi wa Tanzania. Mkulima wa zabibu, Victoria Zablon wa kijiji cha Matumbulu nje ya Jiji la Dodoma akionja sukari ya zao hilo. 

TDL inaamini jitihada za Serikali za kuigeuza Tanzania kuwa nchi ya viwanda zinaweza kufanikiwa  ikiwa wakulima wadogo wanawezeshwa kuzalisha malighafi inayohitajiwa na viwanda.

Baadhi ya wakulima wa zao la zabibu Kijiji cha Matumbulu nje ya Jiji la Dodoma wakiwa na makreti yenye zao hilo baada ya kuvuna tayari kwa kusafirishwa kupelekwa kiwandani kwa ajili ya uzalishaji wa vinywaji.

Meneja Mkuu wa TDL, Devis Deogratius amesema kampuni hiyo kwa sasa inanunua takribani lita milioni 1.2 za mchuzi wa zabibu kwa mwaka kutoka kampuni za CETAWICO na UWAZAMAM, ambazo zinanunua zabibu za wakulima wa ndani  ambapo  inatumia bilioni 3.3 kwa mwaka.

 Mkulima wa zabibu Daniel Ngoima wa Kijiji cha Matumbulu nje ya Jiji la Dodoma  akivuna zao hilo kama alivyokutwa  shambani kwake.

Deogratius ameongeza kuwa, kamouni hiyo imedhamiria kununua malighafi ya ndani katika kipindi chote cha miaka ijayo ambapo kwa sasa inatumia malighafi na huduma za kufanikisha uzalishaji kwa asilimia 80 ambayo ni sawa na shilingi bilioni 46.  
 
TDL imewekeza katika uundaji wa chapa za Kitanzania ambazo ni pamoja na: Imagi, Valeur, Wines Dodoma, Dodoma Rose, Konyagi na Zanzi Cream liqueur ambazo  zimetengenezwa kwa viwango vya ubora kwa  Kimataifa kwa kulenga mahitaji ya makundi mbalimbali katika soko.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news