Wagombea 10 wapeta Musoma, wanne wadunda, mmoja aacha kituko cha mwaka

MSIMAMIZI wa Uchaguzi katika Jimbo la Musoma Mjini,Fidelica  Myovera amesema kuwa jumla ya wagombea 10 kati ya 14 waliochukuwa fomu za Tume  ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kutoka vyama mbalimbali  vya siasa wamerejesha na  kuteuliwa   kuwania nafasi hiyo katika Jimbo la Musoma Mjini.


Mgombea Ubunge wa Jimbo la Musoma Mjini,Vedastus Mathayo (CCM) akipokea barua ya uteuzi kutoka kwa Msimamizi wa Uchaguzi Jjmbo hilo,Fidelica Myovera mjini hapa leo. Picha na Amos Lufungulo/www.diramakini.co.tz

Ni baada ya kukidhi vigezo, huku  wengine kutoka vyama vitatu  wakishindwa kurejesha na mmoja akirejesha,lakini hajakidhi vigezo, anaripoti Amos Lufungulo-Musoma www.diramakini.co.tz

Myovera ameyasema hayo leo wakati akizungumza na waandishi wa habari Mjini Musoma, ambapo pamoja na mambo mengine amesema zoezi la uchukuaji fomu na urejeshaji limefanyika vizuri na kwamba changamoto iliyojitokeza ni Mgombea mmoja kutoka Chama Cha 'AAFP' ambaye alichukua fomu leo na kurejesha leo, muda mfupi kabla ya zoezi hilo kufungwa, huku akiwa hajakidhi baadhi ya vigezo na hivyo kushindwa kuteuliwa.

Amevitaja vyama  10 ambavyo wagombea wake wameteuliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa ni pamoja na ACT Wazalendo, CUF, CHADEMA, NCCR Mageuzi, CCM, CCK, DP, NRA,UDP, ADC.

Kwa upande wake Mgombea Ubunge wa Jimbo la Musoma Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi,Vedastus  Mathayo akizungumza mara baada ya kurejesha fomu  amesema kuwa, iwapo atashinda katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu atahakikisha anashirikiana na wananchi wa Jimbo la Musoma Mjini kutatua changamoto zilizopo ili maendeleo yaweze kuendelea kufanyika kwa kipindi kingine cha miaka mitano.

Mathayo ameongeza kuwa, wananchi wanapaswa kuendelea kumuamini pamoja na chama chake na hivyo wakipe ushindi wa kishindo kwa kuchagua viongozi kuanzia diwani, mbunge pamoja na  Rais Magufuli  kwa ajili ya  kuendelea kuwaletea maendeleo katika nyanja mbalimbali ikiwemo uchumi, na kuimarisha huduma za kijamii.

"Wananachi wa Musoma  Mjini nipo nao pamoja wakati wote, kwa hiyo nasisitiza kuwatumikia kwa moyo wa dhati baada ya kunichagua ili changamoto zilizopo tuweze kuzitatua kwa pamoja tukitekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi kwa kushirikiana na Rais Magufuli kwa miaka mingine mitano ijayo,"amesema.

Nao wgombea walioteuliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kutoka vyama mbalimbali Jimbo la Musoma Mjini  wakizungumza na www.diramakini.co.tz kwa nyakati tofauti  baada ya majina yao kubandikwa wamesema zoezi la uchukuaji fomu na urejeshaji limefanyika vizuri na kwamba, hakuna changamoto zilizojitokeza tangu mchakato huo ulipoanza na kuhitimishwa.

"Zoezi la uchukuaji fomu na urejeshaji  limefanyika vizuri upande wangu sijaona changamoto kama zipo basi  ni ndogondogo na ambazo ni za kibinadamu,lakini kwa ufupi limeenda vizuri,"amesema Julius Mwita mgombea kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here