Hatimaye Klabu ya FC Bayern Munich ya Ujerumani imefanikiwa kutwaa Ubingwa wa German Super Cup dhidi ya Borussia Dortmund katika mchezo wa fainali uliochezwa bila uwepo wa mashabiki uwanjani,anaripoti Mwandishi Diramakini.
Katika mchezo huo ambao ulikuwa na ushindani wa hali ya juu umemalizika kwa FC Bayern Munich kupata ushindi wa magoli 3-2, magoli ya Bayern yamefungwa na Joshua Kimmich na Thomas Muller.
Borussia Dortmund magoli yao mawili yamefungwa na Brandt na Haaland, ushindi huo sasa unamfanya Thomas Muller aandike rekodi ya kuwa mchezaji wa Kijerumani mwenye mafanikio zaidi baada ya kutwaa taji lake la 27 hadi sasa. "Tumepambana kwa ajili ya kombe, tumepata, Mungu asante,"amesema Joshua Kimmich ambaye amekuwa sehemu ya ushindi huo.
"Ushindi huu kwetu ni heshima kubwa sana, haya ndiyo malengo yetu ya kuyaendea mafanikio," amesema Kocha Hansi Flick baada ya kutwaa ubingwa huo.
Katika mchezo huo ambao ulikuwa na ushindani wa hali ya juu umemalizika kwa FC Bayern Munich kupata ushindi wa magoli 3-2, magoli ya Bayern yamefungwa na Joshua Kimmich na Thomas Muller.
Borussia Dortmund magoli yao mawili yamefungwa na Brandt na Haaland, ushindi huo sasa unamfanya Thomas Muller aandike rekodi ya kuwa mchezaji wa Kijerumani mwenye mafanikio zaidi baada ya kutwaa taji lake la 27 hadi sasa. "Tumepambana kwa ajili ya kombe, tumepata, Mungu asante,"amesema Joshua Kimmich ambaye amekuwa sehemu ya ushindi huo.
"Ushindi huu kwetu ni heshima kubwa sana, haya ndiyo malengo yetu ya kuyaendea mafanikio," amesema Kocha Hansi Flick baada ya kutwaa ubingwa huo.