Bodi ya Maziwa yabaini kasoro maziwa ya unga ya Cowbell

Bodi ya Maziwa nchini Tanzania (TDB) imekamata tani tatu za maziwa ya unga ya Cowbell yaliyokuwa yanakaribia kuisha muda wa matumizi yakiwa yameongezwa muda wa matumizi zaidi kwa ajili ya kuyauza, anaripoti Mwandishi Diramakini.
Ukaguzi ukiendelea katika kiwanda hicho kilichopo Keko Chang'ombe katika Manispaa ya Temeke jijini Dar es Salaam. (Picha na Diramakini).

Kaimu Msajili wa Bodi hiyo, Noel Byamungu amesema jijini Dar es Salaam kuwa, wamebaini kitendo hicho katika kiwanda cha Kampuni ya Hawai Limited kilichopo Keko Chang'ombe katika Halmashauri ya Manispaa ya Temeke jijini Dar es Salaam wakiwa katika majukumu yao ya ukaguzi na usimamizi wa kuhakikisha wananchi wanapata maziwa bora nchini.

Byamungu amesema, maziwa hayo yalitakiwa kumaliza muda wake wa matumizi mwezi Juni, Agosti na Oktoba, mwaka huu lakini kiwanda hicho kilifanya kitendo cha kufunga upya maziwa hayo katika vifungashio vipya vinavyoonesha mwisho wa matumizi ya maziwa hayo kuendelea kutumika hadi mwezi Agosti mwaka 2022.

Amesema, watendaji wamewaachia Jeshi la Polisi mkoa wa Kipolisi Temeke ambao ni Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Ahemed Suleiman Mohamed pamoja na Meneja uzalishaji, Ahmed Amanzi kujibu tuhuma zinazowakabili.

Kamishina Msaidizi wa Mkoa Kipolisi Temeke Amon Kakwale amesema tayari wanawashikilia watendaji wa kampuni hiyo kwa hatua za kichunguzi zaidi kabla ya kufikishwa katika mamlaka za kisheria.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news