TBS:Utaratibu wa kukagua magari kutoka nje ya nchi unabadilika Machi 1, 2021

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limewaeleza waagizaji na wauzaji wa magari kutoka nje ya nchi kuwa, kuanzia Machi Mosi, 2021 utaratibu wa kukagua magari kutoka nje ya nchi utafanyika baada ya kuwasili hapa nchini (destination inspector),anaripoti Mwandishi Diramakini. 
Kwa mujibu wa taarifa iliyoonwa na Mwandishi Diramakini kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano wa TBS, Roida Andusamile, magari yote yatakayosafirishwa kuanzia tarehe tajwa hapo juu yatakaguliwa katika Bandari ya Dar es Salaam.

"Kwa sasa TBS inakagua magari kutoka nje ya nchi kupitia mawakala watatu kutoka Japan na mmoja kutoka Dubai ambao mikataba yao itakoma hivi karibuni. Hivyo vyeti vya ukaguzi vitatolewa na mawakala tajwa kwa magari yatakayosafirishwa kuanzia Machi Mosi, 2021 havitatambuliwa na TBS,"TBS imeeleza.

Aidha, kwa mujibu wa TBS magari yatakayopimwa bandarini na kutokidhi matakwa ya kiwango yatahitaji kufanyiwa matengenezo nje ya bandari na kisha kuletwa na kupimwa tena kwenye yadi ya UDA mkabala na Bandari ya Dar es Salaam.

"Shirika litaendelea kuhakikisha kuwa, magari yote yaliyotumika na kuingizwa nchini yanakidhi matakwa ya kiwango cha magari yanayotumika,"imeongeza TBS.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news