Mahakama ya Tanzania yatoa orodha ya 'Mawakili Wasiojulikana'


Imebainika kuwa kuna idadi kubwa ya Mawakili ambao mpaka kufikia tarehe ya tangazo hili hawajahuisha taarifa zao binafsi na kuweka maelezo muhimu katika akuanti zao kwenye mfumo wa mawakili Tanzania unaojulikana kama Tanzania Advocate Management System (TAMS). Mawakili hawa wako wapi,kumepelekea kutokuwepo taarifa zao kwenye mfumo wa Mawakili Tanzania pamoja na Kanzidata ya Mawakili. Aidha, uwepo wa taarifa sahihi za Wakili anayehusika katika Chama cha Wanasheria Tanganyika na Ofisi ya Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania kunawapa fursa wadau wote na wananchi kwa ujumla kuwafahamu Mawakili walioruhusiwa kufanya kazi ya Uwakili, hivyo kama Mahakama ya Tanzania kupitia Ofisi ya Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania inauntangazia umma kwamba mtu yeyote ambaye ana taarifa za Wakili au anafahamu chochote kuhusu yeyote aliyeorodheshwa katika orodha iliyowekwa hapa chini tafadhali anaombwa kutoa taarifa hizo kupitia anuani ya barua pepe rhc@judiciary.go.tz au unaweza kupiga simu ya mkononi nambari 0739303038. Kwa maelezo zaidi kuhusu tangazao la 'Mawakili Wasiojulikana' tafadhali tembelea tovuti yetu www.judiciary.go.tz na kwenye blogu yetu Tanzaniajudiciary.blogspot.com.



Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

1 Comments

Previous Post Next Post

International news