Rais Samia atengua uteuzi wa DC Msulwa, DED Sheilla Lukuba

NA MWANDISHI DIRAMAKINI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan leo tarehe 15 Juni, 2021 ametengua uteuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Bw. Bakari Msulwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Wilaya hiyo, Bi. Sheilla Lukuba kwa kushindwa kusimamia Wafanyabishara wadogo wadogo (Wamachinga) mkoani Morogoro.

Mhe. Rais Samia ametangaza hatua hiyo wakati akihutubia vijana wa Mkoa wa Mwanza na mikoa jirani waliowawakilisha vijana wote nchini.

Amesema, amesikitishwa na kitendo cha Asakri Mgambo katika eneo la Kituo cha Mabasi Morogoro kuwanyanyasa Wafanyabishara wadogo maarufu kama Wamachinga wanaofanya baishara nje ya Kituo hicho.

Mhe. Rais amesema kitendo cha kunyanyaswa wafanyabishara hao si cha kiungwana na hakikubali kamwe.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news