Ajali yaua wafanyakazi watano wa TRA

SONGWE,Watu Watano Wafanyakazi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA wamefariki dunia kutokana na ajali ya gari aina ya Landcruiser yenye nambari za Usajili STL 8825 Mali ya Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA ambalo liligonga Lori aina ya FUSO yenye nambari za usajili T 586 ANE.
Ajali hiyo imetokea katika kijiji cha Hanseketwa Wilayani Mbozi Mkoani Songwe majira ya saa 11 alfajiri leo Agosti 23,2021.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe, Janeth Magomi amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo.Picha zaidi soma hapa>>>

Wafanyakazi hao ni kikosi kazi cha Fast Track na wamefariki wakiwa wanafukuzana na gari walilokua wanadhani limebeba bidhaa za magendo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news