Katibu Mkuu CCM Taifa akiri kupokea barua ya kujiuzulu Spika Ndugai

NA GODFREY NNKO

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Daniel Chongolo amethibitisha kupokea barua ya kujiuzulu kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Job Ndugai.

Hayo yamebainishwa kupitia taarifa iliyotolewa leo Januari 6,2022 na Afisa Habari kutoka Ofisi ya Katibu Mkuu CCM,Said Said Nguya.

"Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ndugu Daniel G. Chongolo leo tarehe 6 Januari, 2022 amethibitisha kupokea barua ya Mheshimiwa Job Yustino Ndugai (Mb) ya kujiuzulu nafasi ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

"Katibu Mkuu ameeleza kuwa, mchakato wa kumpata Spika mwingine baada ya nafasi hiyo kubaki wazi unaendelea,"imeelezea taarifa hiyo.
Katibu Mkuu CCM Taifa, Daniel Chongolo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news