Tanzania, Ufaransa zasaini mikataba sita ya makubaliano

NA GODFREY NNKO

SERIKALI za Tanzania na Ufaransa leo zimetia saini jumla ya mikataba sita ya makubaliano kwa nia ya kuendeleza uhusiano baina ya nchi hizo mbili.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, akishuhudia utiaji saini wa mikataba ya ushirikiano katika sekta mbalimbali kati ya Tanzania na Ufaransa iliyosainiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula pamoja na Waziri wa Biashara wa Ufaransa, Frank Reicster katika mji wa Brest nchini Ufaransa leo Ijumaa Februari 11, 2022. (Picha na Ikulu).

Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Februari 11,2022 kutoka mjini Brest nchini Ufaransa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais (Ikulu), Bi.Zuhura Yunus.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan pamoja na Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa katika mkutano wa 'One Ocean Summiť uliofanyika mjini Brest, Ufaransa.
Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan akiwa katika mazungumzo na Waziri wa Biashara wa Ufaransa, Frank Reicster kabla ya kushuhudia utiaji saini wa mikataba ya ushirikiano katika sekta mbalimbali katika Tanzania na Ufaransa katika mji wa Brest nchini Ufaransa leo tarehe 11 Februari, 2022.

Amesema kuwa, Rais Samia ameshuhudia utiaji saini wa baadhi ya mikataba na makubaliano baina ya Waziri wa Fedha na Mipango wa Tanzania, Mwigulu Nchemba na Waziri wa Biashara wa Ufaransa Frank Reister.

Miongoni mwa makubaliano hayo ni mkataba wa mkopo wa masharti nafuu wenye thamani ya Euro milioni 178 kwa ajili ya kugharamia mradi wa ujenzi wa barabara wa mabasi yaendayo haraka.

Serikali hizo pia zimesaini mkataba wa mkopo wa masharti nafuu wenye thamani ya Euro milioni 80 ili kuimarisha Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania kufikia malengo ya kutoa mikopo ya muda mfupi na mrefu kvva sekta ya kilimo. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akishuhudia Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Mwigulu Nchemba akiweka saini moja ya mikataba ya ushirikiano wa kimaendeleo katika Nyanja mbalimbali kati ya Tanzania 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, akishuhudia utiaji saini wa mikataba ya ushirikiano katika sekta mbalimbali kati ya Tanzania na Ufaransa iliyosainiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula pamoja na Waziri wa Biashara wa Ufaransa Frank Reicster katika mji wa Brest nchini Ufaransa leo Ijumaa Februari 11, 2022.

Aidha Rais Samia ameshuhudia utiaji saini wa mikataba mingine ya ushirikiano baina ya nchi hizo iliyosainiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula kwa niaba ya serikali.

Pia serikali za Tanzania na Ufaransa zimesaini tamko la dhamira ya kushirikiana katika eneo la uchumi wa buluu na usalama wa bahari.

Wakati huo huo, Rais Samia ameyasihi mataifa yote kuheshimu makubaliano na maazimio waliyotia saini, kama wajibu wa kuchukua hatua madhubuti katika kulinda bahari.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, akishuhudia utiaji saini wa mikataba ya ushirikiano katika sekta mbalimbali kati ya Tanzania na Ufaransa iliyosainiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula pamoja na Waziri wa Biashara wa Ufaransa Frank Reicster katika mji wa Brest nchini Ufaransa leo Ijumaa Februari 11, 2022.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali walioalikwa na mwenyeji wao Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa, mjini Brest katika mkutano unaojadili kuhusu Raslimali Bahari Duniani leo tarehe 11 Februari, 2022.

Rais Samia aliyasema hayo wakati wa kuhutubia mkutano wa siku tatu ujulikanao kama 'One Ocean Summiť mjini Brest, Ufaransa, ulioandaliwa na Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news