Serikali imeendelea kuimarisha hatua za kuzuia ugonjwa wa Ebola kuingia nchini huku ikithibitisha kuwa hadi sasa hakuna mgonjwa aliyegundulika Tanzania, licha ya kuwepo kwa mlipuko wa ugonjwa huo katika nchi jirani za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Uganda.

Akizungumza na waandishi wa habari Juni 18,2026 jijini Dodoma , Waziri wa Afya, Mohamed Mchengerwa, amesema mifumo ya ufuatiliaji, utambuzi na udhibiti wa ugonjwa huo imeimarishwa ili kuhakikisha usalama wa afya za Watanzania unaendelea kulindwa wakati wote.
Amesema Serikali ilichukua hatua za mapema mara baada ya kutangazwa kwa mlipuko huo katika nchi jirani, ikiwemo kutoa Mwongozo wa Wasafiri Na. 17 wa Mei 19, 2026, unaobainisha tahadhari na masharti ya kiafya kwa wasafiri wote wanaoingia nchini.
“Tunaendelea kuwafahamisha wananchi kuwa hadi sasa nchi yetu haina mgonjwa wa Ebola na hali ya usalama wa afya nchini iko vizuri. Serikali imejipanga kikamilifu kuzuia, kugundua mapema na kudhibiti tishio lolote la ugonjwa huo,” amesema Mchengerwa.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo












