Diamond Platnumz atoa milioni 10/- kuendeleza vituo vya Madrasa Dodoma

NA DIRAMAKINI

KAMPUNI ya Wasafi Media imetoa shilingi milioni 10 kwa ofisi Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania (BAKWATA) Mkoa wa Dodoma ili kuendeleza vituo vya mafunzo ya Kiislam (Madrasa).

Akizungumza leo Aprili 27,2022 jijini Dodoma kwenye tukio la la fadhila za Ramadhani Iftar lililofanyika katika viwanja vya Bunge jijini humo, Mkurugenzi Mkuu wa Wasafi Media, Nasibu Abdul (Diamond Platnumz) amesema fedha hizo zitakwenda kusaidia kununua vitabu vya kusomea,busati na mikeka kwa ajili ya kuswalia.
Bw.Nasibu amekabidhi fedha hizo kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt.Tulia Ackson ambapo Spika amemkabidhi Sheikh wa Mkoa wa Dodoma, Mustapha Rajabu.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news