Wenye malalamiko kuhusu kurejeshewa mifugo iliyokamatwa hifadhini yaleteni wizarani-Mhe.Masanja

NA HAPPINESS SHAYO-WMU

NAIBU Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) amewataka wananchi wanaoilalamikia Serikali kuhusu kurejeshewa mifugo iliyokamatwa hifadhini kuwasilisha maombi yao Wizara ya Maliasili na Utalii ili yafanyiwe kazi.

Ameyasema hayo leo Bungeni jijini Dodoma alipokuwa akijibu swali na Mbunge wa Kisesa, Mhe. Luhaga Mpina.

“Endapo kuna wananchi ambao mifugo yao ilikamatwa na mahakama kuamuru kurejeshwa mifugo yao na hawajarejeshewa wawasilishe malalamiko yao Wizara ya Maliasili na Utalii ili yashughulikiwe,” Mhe. Masanja amesisitiza.

Aidha, amewataka wananchi hususan wafugaji kuacha kuingiza mifugo kwenye maeneo ya Hifadhi kwani kwa mujibu wa Sheria ya Uhifadhi Wanyamapori namba 5 ya mwaka 2009 ni kosa kuingiza na kuchunga mifugo ndani ya hifadhi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news