'Tupo tayari kuhesabiwa sisi kama Viongozi wa Dini pamoja na Waumini wetu'


NA DIRAMAKINI

MKUTANO wa Kamati ya Amani na Jumuiya ya Maridhiano kuhusu Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022. 

Mkutano huu umefanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam ambapo Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson alikuwa mgeni rasmi. 
Katika mkutano huu; Viongozi wa Dini wameahidi kushiriki kwenye Sensa pamoja na kuwaelimisha na kuwahamasisha waumini wao kujitokeza kuhesabiwa.
"Tupo tayari kuhesabiwa sisi kama Viongozi wa Dini pamoja na Waumini wetu," wamesema kwa kauli moja Viongozi wa Dini ambao ndio wajumbe wa Kamati ya Amani na Jumuiya ya Maridhiano.

Sensa ya Watu na Makazi itafanyika tarehe 23 Agosti, 2022. Sensa kwa Maendeleo, Jiandae Kuhesabiwa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news