NA STEVEN NYAMITI-WM
SERIKALI imewataka wachimbaji na wafanyabiashara wa madini nchini kusafisha dhahabu katika viwanda vya ndani badala ya kuuza malighafi kwenye viwanda vya nje.
Rai hiyo imetolewa leo Julai 7, 2022 na Waziri wa Madini, Dkt. Doto Biteko alipotembelea kiwanda cha kusafisha dhahabu cha Geita Gold Refinery (GGR) cha mkoani Geita.

"Ni muhimu sasa dhahabu tunayoichimba wenyewe iweze kusafishwa hapa iende ikiwa bidhaa ya mwisho,"amesisitiza.
Aidha, Dkt.Biteko amesema, kiwanda cha GGR kitatengemeza ajira kwa Watanzania pamoja na kulipa kodi husika ili Serikali iweze kukusanya mapato.



Amesema, kiwanda hicho ni mkombozi wa wachimbaji na wafanyabiashara wa madini kwa mkoa ili waweze kusafisha dhahabu katika ubora wa kimataifa.
Hadi sasa Serikali ina viwanda vya kusafisha dhahabu katika mkoa wa Mwanza na Dodoma ambavyo wachimbaji na wafanyabiashara wa madini ndani na nje nchi hupeleka madini kwa ajili ya kusafishwa.
0 Comments