Kamati ya Wakuu wa Nchi na Serikali ya Umoja wa Afrika ya Mabadiliko ya Tabianchi imeiteua Tanzania kuwa mwenyeji wa kituo cha mafunzo ya vijana kuhusu masuala ya mazingira na mabadiliko ya tabianchi.
Hayo yamesemwa mwishoni mwa wiki na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Richard Muyungi wakati akihutubia katika tukio la iftar maalum aliyoiandaa kwa wadau wa mazingira na kufanyika katika Chuo cha Mazingira, Mabadiliko ya Tabianchi na Maendeleo Endelevu kilichopo Bunju jijini Dar es Salaam.


Amesema kamati hiyo imeiteua Tanzania kuwa mjumbe wa kudumu kupitia mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi na Serikali Barani Afrika uliofanyika Addis Ababa, Ethiopia tarehe 14-15 Februari, 2026 na kuhudhuriwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Ameeleza kuwa kituo hicho kitawasaidia Watanzania hususani vijana kuweza kujifunza fursa mbalimbali zilizopo katika sekta ya mazingira na kuongeza kupanua wigo wa ushiriki wa Tanzania katika mijadala mbalimbali ya kimataifa.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo



















