*Lengo ni kurahisisha upatikanaji wa huduma
NA MWANDISHI WETU
MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), unatarajia kufanya maboresho mbalimbali kwenye huduma inazozitoa kwa lengo la uimarishaji na upatikanaji wa huduma bora kwa wanachama wake.

Alielezea maboresho hayo yatauwezesha Mfuko kuwa na taarifa sahihi za wanufaika na mfumo madhubuti wa utambuzi wa wanachama, kuimarisha ubora wa upatikanaji wa huduma, kuondoa usumbufu na kukinga afya za wanufaika.
“Maboresho haya pia yanakwenda kuondoa malalamiko kutoka kwa wadau kutokana na mapungufu katika kitita cha mafao kinachotumika hivi sasa kwa kuwa tunakwenda kuhuisha Kitita cha Mafao kwa kuzingatia Mwongozo wa Tiba nchini (STG), Orodha ya Dawa Muhimu ya Taifa (NEMLIT), Sheria ya Mfuko na Mapendekezo ya Taarifa ya Tathmini ya Uhai na Uendelevu wa Mfuko na kuboresha Kanuni za Mfuko,” alisema Bw. Mapunda.

“Mfuko utaweka utaratibu wa uchangiaji kwa awamu kabla ya kuanza kupata huduma lengo ni kuweka unafuu katika uchangiaji kwa wananchi ili wajiunge na bima ya afya, kuwezesha kuwasilisha taarifa ikiwemo michango kwa njia ya kieletroniki kwa kuimarisha portal ya waajiri na kuendelea kuwezesha wanachama kupata taarifa muhimu kupitia simu zao za mkononi,” alisema Bw. Mapunda.

“Ndugu zangu mtakubaliana na mimi kuwa tunauhitaji huu Mfuko ili utuhudumie lakini kumekuwepo na wimbi kubwa la udanganyifu, niwaombe sana kila mmoja awe mlinzi wa huduma zinazotolewa na Mfuko ili uzidi kuwa imara zaidi,” alisema Bw. Muhimbi.
Akizungumzia Watoa Huduma amewataka waendelee kutoa huduma bora kwa wanachama na kujiepusha na vitendo vya udanganyifu ili kuwezesha Mfuko kulipa madai halali lakini pia kuwa mabalozi wa kutoa taarifa sahihi na sio kuelekeza lawama kwa Mfuko pale inapoonekana huduma fulani haipo.
“Wanachama niwaombe sana kila mmoja ahakikishe kadi yake matibabu haitumiki na mtu mwingine kwani kwa kufanya hivyo ni sawa na kuhujumu Mfuko huu lakini pia kwa Waajiri wahakikishe wanawasilisha michango ya Watumishi wao kwa wakati ili kuepukana na usumbufu kwa wafanyakazi na wategemezi wao kukosa huduma kutokana na kukosekana kwa michango,” alisisitiza Bw. Muhimbi.

“Mfuko uko imara sana na kwa sasa tunajivunia sana uimarishaji wa huduma ambao umefanywa na Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Hassan Suluhu hususan kwa kuweka vifaa tiba vya kisasa katika hospitali mbalimbali nchini ambayo inarahisisha zaidi upatikanaji wa huduma kwa wanachama wetu hivyo kama Mfuko tunaendelea kuunga mkono juhudi za Serikali na kuhakikisha tunawafikia wananchi wengi zaidi ili wajiunge na Mfuko,” alisema Bw. Konga.