Tanzania, Oman kuongeza maeneo ya ushirikiano

NA MWANDISHI WETU

SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Oman zimeahidi kuongeza maeneo mapya ya ushirikiano katika sekta za uwekezaji, elimu, uvuvi na utamaduni.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Balozi wa Oman nchini Mhe. Saudi Hilal Al Sidhani katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

Ahadi hiyo imetolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb.) alipokutana kwa mazungumzo na Balozi wa Oman nchini Mhe. Saudi Hilal Al Sidhani katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

Waziri Mulamula amesema kuwa ni wakati sasa kwa mataifa hayo mawili kuongeza ushirikiano katika sekta za uwekezaji, elimu, uvuvi na utamaduni kwa maendeleo ya mataifa yote mawili.

Nae Balozi wa Oman nchini, Mhe. Al Sidhani amesema kuwa Oman ipo tayari wakati wote kuwekeza katika maeneo yenye fursa hapa Tanzania.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akimkaribisha Balozi wa Oman nchini Mhe. Saudi Hilal Al Sidhani katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

“Naomba endapo Tanzania mtaona maeneo mapya ya ushirikiano hususan fursa za uwekezaji na biashara msisite kutushirikisha tukajadiliana na kuitekeleza azma hiyo kwa maslahi ya pande zote mbili,” amesema Balozi Al Sidhani.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news