UCHAGUZI KENYA KAMA FAMILIA YA KAMBALE KILA MTU ANA NDEVU

NA WANGWE JR

UHURU wa kila mtu kutoa matokeo ya uchaguzi umedhihirisha aibu na fedheha kwa wapenda demokrasia na wachambuzi wa masuala ya siasa barani Afrika na Duniani kote. 

Tume ya Uchaguzi ndio inapaswa kutoa takwimu ili kuepusha mikanganyiko isiyo na tija.

Upande mwingine mshindi wa Ubunge wa Jimbo la Kimilili, Bwana Didmus Barasa amedaiwa kumuua msaidizi wa aliyekuwa mshindani wake katika kinyang'anyiro cha Ubunge wa jimbo hilo. 

Hii ndio maana ya familia ya Kambale yaani kila mmoja ana ndevu, hakuna kuheshimu sheria.

Jioni hii kituo cha kuhesabia kura cha Kirinyaga kimevamiwa na wafuasi wa wanasiasa Anne Waigiru na mwenzie Wangui Ngirici. 

Yanayoendelea ni mfano mbaya ambao unapaswa kuchukuliwa kama somo na nchi nyingine ili kuepusha uhuni kutamalaki katika mawanda ya Demokrasia hapa Afrika.

Mchakato wa Uchaguzi nchini Kenya ni mfano mbaya usiopaswa kuigwa hata punje, ni kama Familia ya Kambale kila mmoja anafanya anavyojisikia.


Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news