Waziri Prof.Mkenda aishirikisha Iran jambo muhimu kuhusu elimu

NA MATHIAS CANAL-WEST

WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe Prof. Adolf Mkenda (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Tanzania, Mhe Alvandi Hossein pamoja na Rais wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Al-Mustafa (Al-Mustafa International University) cha nchini Iran, Dkt Ali Abbasi.
Katika mazungumzo hayo Waziri Mkenda na wageni hao kutoka Iran, wamekubaliana kuendeleza ushirikiano kwenye taasisi za elimu ya juu katika masuala ya Teknolojia, Sayansi, na Elimu ujuzi.
Waziri Mkenda amemuomba Balozi huyo kutoa ufadhili wa masomo kwa wanafunzi wa elimu ya juu na kubadilishana utaalamu baina ya Vyuo Vikuu vya hapa nchini na Iran ili kuongeza wigo wa ujuzi kwa pande zote mbili.
Kadhalika, Waziri Mkenda amemueleza Balozi huyo wa Iran kuwa Tanzania inafanya mapitio ya Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014 na mabadiliko ya mitaala ili kuongeza ubora wa elimu na mafunzo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news