Qatar yaweka historia kuwa nchi ya kwanza mwenyeji kuondolewa

NA DIRAMAKINI

QATAR imekuwa nchi ya kwanza kuandaa Kombe la Dunia la Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) 2022 kuondolewa baada ya michezo yake miwili ya kwanza kufungwa ikiwemo mabao 3-1 yaliyofungwa na Senegal siku ya Ijumaa.

Picha na Sorin Furcoi/Al Jazeera.

Kihisabati haiwezekani kwa wenyeji wa Kombe la Dunia la 2022 kuwa moja ya timu mbili za juu katika Kundi A na kufika kwenye raundi inayofuata ingawa bado kuna hatua moja zaidi ya makundi.

Uholanzi na Ecuador kila moja ilishinda mechi zao za kwanza za michuano hiyo, Ecuador iliifunga Qatar 2-0 na kufungwa 1-1 Ijumaa.

Kila moja ina alama nne na Senegal ina alama tatu baada ya ushindi wake dhidi ya Qatar. Hata kama Qatar itaifunga Uholanzi siku ya Jumanne itakuwa na alama zisizozidi tatu.

Senegal walienda muda wa mapumziko wakiwa na mabao yao mawili muhimu. Boulaye Did alifunga dakika ya 41 kisha Famara Diedhiou akafunga bao la kufutia machozi dakika tatu tu baada ya kipindi cha mapumziko.

Mohammed Muntari aliifungia Qatar dakika ya 78, lakini Senegal walisawazisha mchezo kwa Bamba Dieng dakika ya 84.

Qatar lilikuwa taifa la kwanza kufuzu kwa Kombe la Dunia la 2022 moja kwa moja kama wenyeji waliposhinda zabuni ya kuandaa mashindano hayo.

Pia ilikuwa ni mara yao ya kwanza kuonekana kwenye mashindano hayo wakiwa hawajawahi kufuzu katika fainali, lakini kuondolewa kwake baada ya michezo miwili kumeonekana kumekatisha tamaa nchi hiyo ambayo ilikuwa inajiandaa kwa Kombe la Dunia kwa zaidi ya muongo mmoja.

Miundombinu ya timu ya taifa ya soka ya Qatar ilijengwa kwa ajili ya mashindano hayo na timu ya taifa ilicheza katika matukio kama vile North American Gold Cup ili kujiandaa kwa Kombe la Dunia.

Qatar inaungana na Afrika Kusini kama nchi pekee zilizotolewa kwenye Kombe la Dunia katika hatua ya makundi. Afrika Kusini iliifunga Mexico wakati wa kufungua Kombe hilo la Dunia, lakini ushindi wake dhidi ya Ufaransa katika mechi ya mwisho ya kundi haukutosha kusonga mbele huku Mexico ikisonga mbele kupitia tofauti ya mabao.

Inadaiwa kuwa, licha ya maandalizi mazuri yaliyofanywa na Qatar kwa ajili ya kombe hilo, kuna mamilioni ya watu duniani ambao hawajafurahishwa na wanayodai kutokidhi matakwa yao,ingawa asilimia kubwa ya watu wanapongeza uamuzi sahihi unaochukuliwa na taifa hilo kulinda maadili na heshima yake.

Kulingana na Idara ya Haki ya Marekani, maafisa wengi wa FIFA walipokea hongo ili kuipigia kura Qatar kama mwenyeji wa michuano hiyo.

Na baada ya Qatar kupata zabuni ya Kombe la Dunia, unyanyasaji wake mbaya kwa maelfu ya wafanyakazi wahamiaji ambao walisaidia kujenga viwanja vya michezo, inatajwa kuwa ishara mbaya katika mashindano pamoja na rekodi inayotajwa kuwa mbaya ya haki za binadamu ya nchi hiyo.

Aidha, kilichokwaza wengi zaidi ni baada ya FIFA kuja na uamuzi mgumu ambapo imeandaa taratibu zinazotumika viwanjani wakati wa michuano ya Kombe la Dunia 2022.

Taratibu hizo ambazo zinatajwa kuwa ni ngumu kuliko miaka ya nyuma ni pamoja na mashabiki kutakiwa kuvaa vizuri na kujisitiri hasa maeneo nyeti ya miili yao, pia wameaswa kuwa michoro ya mwilini kwa maana ya tatoo haitakiwi kuonekana kwa kuwa, hiyo sio nguo.

Pia FIFA inaelekeza kuwa, mtu yeyote atakayeingia kutazama mechi asiwe amelewa pombe au dawa za kulevya,kwani hilo ni kosa kisheria.

Aidha, chupa, vikombe, makopo au vitu vyovyote vinavyoweza kurushwa na kuumiza mtu haviruhusiwi viwanjani, pia vyakula vya aina zote haviruhusiwi labda tu awe amebebewa mtoto.

Mbali na hayo, kupitia mechi zote ambazo zitadumu kwa siku 28, vuvuzela zimepigwa marufuku na vitu vingine kama maputo havitoruhusiwa ikiwemo aina yoyote ya ishara zinazohamasisha mapenzi ya jinsia moja.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news