Hawa ndiyo waliozuiwa matokeo ya Darasa la Saba kwa tuhuma za udanganyifu

NA DIRAMAKINI

WATAHINIWA 540 wanaotoka katika vituo sita vya Joylanda, Castle hill, Green Acress, Maktaba, Great Vision na Mtendeni jijini Dar es Salaam wamezuiwa matokeo ya darasa la saba baada ya kubainika kufanya udanganyifu.
Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) limeeleza leo Desemba Mosi, 2022 kuwa
matokeo ya watahiniwa hao yanazuiwa hadi uchunguzi juu ya tuhuma hizo utakapokamilika.

“Wakibainika kufanya udanganyifu matokeo yao yatafutwa kwa mujibu wa kifungu Na. 4(8) cha Kanuni za Mitihani 2016 na endapo hawatabainika kufanya udanganyifu watapewa matokeo yao".

Pia NECTA linazuia matokeo ya watahiniwa 179 ambao waliugua au walipata matatizo na kushindwa kufanya mitihani kwa masomo yote au baadhi ya masomo.

“Watahiniwa hudika watapewa fursa nyingine ya kurudia kufanya mtihani wa Kumaliza elimu ya msingi (PSLE) mwaka 2023 kwa mujibu wa kifungu 32(1) cha Kanuni za Mitihani;

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news